Mwalimu ahukumiwa kunyongwa hadi kufa Bukoba
Walimu hao walishitakiwa kwa kumuua kwa kukusudia Sperius Eradius aliyekuwa mwanafunzi wa darasa la tano katika shule hiyo mwishoni mwa mwaka 2018.
Upande wa Jamhuri uliwasilisha mashahidi tisa katika kesi hiyo iliyosikilizwa kwa mwezi mmoja na Jaji Lameck Mlacha, ilianza Februari 6, 2019.
Inadaiwa walimu hao walitenda kosa la kumuadhibu kwa kipigo mwanafunzi Sperius Eradius kwa madai kuwa aliiba mkoba wa mwalimu ukiwa na fedha.
Mwalimu ahukumiwa kunyongwa hadi kufa Bukoba
Reviewed by Zero Degree
on
3/06/2019 11:50:00 AM
Rating:
