Loading...

ACT Wazalendo yapata pigo mkoani Kigoma.

CHAMA cha ACT Wazalendo kimeendelea kupata pigo la kukimbiwa na viongozi baada ya aliyekuwa Katibu Mwenezi wa chama hicho wilayani Kasulu mkoani Kigoma, Danford Joel kukihama chama hicho na kujiunga na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).

Akizungumza kwenye ofisi za Chadema mkoa wa Kigoma, Joel alisema ameamua kukihama chama hicho na kurudi Chadema baada ya kuona yale aliyokuwa akiyapigania hayatekelezwi.

Alisema wakati wanajiunga ACT yapo mambo waliaminishwa na kukiona chama hicho kitakuja kuwa mkombozi wa Watanzania, lakini akadai kwa sasa imani hiyo imepotea, kwani taratibu na uendeshaji wa chama umebaki kwa mtu mmoja mithili ya kampuni, huku kukiwa hakuna ushirikishwaji wa viongozi wa ngazi za wilaya.

Alidai kwa sasa maeneo mengi ya mkoa wa Kigoma, ikiwemo Kasulu ambako walipigania chama hicho kimeanza kupoteza nguvu na mvuto wake na kubaki na nguvu kubwa katika Manispaa ya Kigoma Ujiji.

Source: Habari Leo
ZeroDegree.
ACT Wazalendo yapata pigo mkoani Kigoma. ACT Wazalendo yapata pigo mkoani Kigoma. Reviewed by Zero Degree on 12/31/2016 10:16:00 AM Rating: 5

Powered by Blogger.