Loading...

VIDEO: Jinsi Arsenal walivyopigana kiume kujiepusha na aibu ya kichapo cha goli 3 bila.

Michezo ya Ligi Kuu England msimu wa 2016/2017 bado inaendelea kuchezwa katika ardhi ya England, usiku wa January 3 2017 ilichezwa michezo mitatu ya Ligi Kuu England, moja kati ya mchezo uliyochezwa usiku wa January 3 AFC Bournemouth walikuwa wenyeji wa Arsenal katika uwanja wa Goldsands.

Katika mchezo huo Arsenal wamenusurika kupoteza mchezo huo, hiyo inatokana na kuruhusu magoli matatu kwa bila hadi dakika ya 69, Arsenal walirudi mchezoni na kupata goli la kwanza dakika ya 70 kupitia kwa Alex Sanchez, Lucas Perez dakika ya 75 na Oliver Giroud dakika ya 90.


Msimamo wa EPL baada ya mechi za January 3 2017



Kwa upande wa AFC Bournemouth magoli yalifungwa na Charlie Daniels dakika ya 17, Callum Wilson dakika ya 21, Ryan Fraser dakika ya 58, kama hukupata nafasi ya kucheki game yenyewe nimekuwekea magoli yote sita hapa.

ZeroDegree.
VIDEO: Jinsi Arsenal walivyopigana kiume kujiepusha na aibu ya kichapo cha goli 3 bila. VIDEO: Jinsi Arsenal walivyopigana kiume kujiepusha na aibu ya kichapo cha goli 3 bila. Reviewed by Zero Degree on 1/04/2017 12:42:00 PM Rating: 5

Powered by Blogger.