Loading...

Hii ndio ''First Eleven'' ya pekee iliyopangwa na Ronaldo de Lima


Linapokuja suala la kwamba ni Ronaldo yupi bora zaidi katika soka, walio wengi kwa sasa wanamtambua Cristiano Ronaldo kama mtu aliyelipoteza jina la Mabrazili huyo.


Hata hivyo, yeye kama yeye (Ronaldo) amemuweka pembeni Mreno (C. Ronaldo) huyo ambaye ni mshindi wa tuzo ya Ballon D'Or mara nne kwenye kikosi chake bora cha miaka yote.

Ronaldo, kama wajina wake C. Ronaldo ambaye pia aliichezea Real Madrid kama mshambuliaji, yeye binafsi amempa nafasi Lionel Messi kwenye kikosi chake kama kiungo.

Badala yake, mshindi huyo wa Kombe la Dunia mwaka 2002 amejichagua mwenyewe kama mshambuliaji katika mfumo wa 4-4-2 pembeni ya mbrazili mwenzake, Pele.

Katika maisha ya soka, Ronaldo, alifanikiwa kushinda tuzo ya Ballon d'Or mara mbili.


Golikipa wa sasa wa Juventus, Gianluigi Buffon amechaguliwa kunza kikosini, pamoja na mshindi wa Kombe la Dunia mwaka 2006, Fabio Cannavaro na mkongwe wa AC Milan, Paolo Maldini kuwekwa katika nafasi ya beki wa katikati.

Ronaldo amewachagua wachezaji wanne wa Brazili, wanne wa Italia, wawili wa Argentina na Mfaransa mmoja katika kikosi chake
Ronaldo anawachagua wenzake toka Brazil, Cafu na mtaalamu wa mipira ya adhabu, Roberto Carlos katika nafasi ya beki wa pembeni.

Wakati Cristiano Ronaldo anaachwa nje, meneja wake wa Real Madrid, Zinedine Zidane yuko ndani ya kikosi hicho katika nafasi ya kiungo pamoja na Andrea Pirlo.

Uhasimu kati ya Brazil na Argentina umewekwa pembeni katika nafasi ya winga, baada ya Diego Maradona na Lionel Messi kupewa kibarua cha kuwatengenezea mipira Ronaldo na Pele.



Hii ndio ''First Eleven'' ya pekee iliyopangwa na Ronaldo de Lima Hii ndio ''First Eleven'' ya pekee iliyopangwa na Ronaldo de Lima Reviewed by Zero Degree on 10/08/2017 02:21:00 AM Rating: 5

Powered by Blogger.