Loading...

Idadi ya majeruhi Chelsea yazidi kuongezeka


Kiungo wa klabu ya Chelsea, N'Golo Kante alipata majeraha katika paja wakati Ufaransa ilipoivaa Bulgaria kwenye michuano ya kufuzu kucheza Kombe la Dunia.

Kante alianza na kikosi cha kwanza akiwa kama kiungo wa kati katika mechi hiyo ambayo ilimalizika kwa Ufaransa kuibuka na usindi wa goli 1-0, lakini nafasi yake ilichukuliwa na Adrien Rabiot baada ya dakika 33 tu za mchezo.

Ikumbukwe kwamba, Chelsea walimsajili Danny Drinkwater akiwa na majeraha kwenye shavu la mguu, hivyo kumfanya meneja Antonio Conte na uchaguzi mdogo katika safu ya kiungo.

Baada ya pumziko hili la michuano ya kimataifa, Chelsea watasafiri kuifuata Crystal Palace siku ya Jumamosi, hata hivyo, haijafahamika kama Kante ataukosa mchezo huo.
Idadi ya majeruhi Chelsea yazidi kuongezeka Idadi ya majeruhi Chelsea yazidi kuongezeka Reviewed by Zero Degree on 10/08/2017 10:11:00 AM Rating: 5

Powered by Blogger.