Loading...

Ronaldo, Pogba kutengeneza historia UEFA


Moja ya mechi kali na ya kihistoria leo kwenye ligi ya mabingwa Ulaya ni kati ya Manchester United dhidi ya Juventus, itakayopigwa kwenye dimba la Old Traford ambapo mbali na kumkaribisha Cristiano Ronaldo lakini kutakuwa na matukio mbalimbali.

Mchezo huo ambao ni wa kwanza kwa timu hizo kukutana tangu mwaka 2003 utashuhudia historia mbalimbali zikiwekwa.

Paul Pogba

Mchezaji ghali zaidi katika kikosi cha Manchester United Paul Pogba, ambaye alinunuliwa kutoka Juventus kwa dau la rekodi ya dunia €105m mwaka 2016 atakuwa anakutana na timu yake ya zamani pamoja na kukabiliana na nyota mwenzake wa Ufaransa.

Ronaldo dhidi ya Man United
Hii ni mara ya pili kwa Cristiano Ronaldo kurejea Old Traford akiwa kama mpinzani baada ya kufanya hivyo akiwa na Real Madrid na sasa Juventus.

Baada ya jana kufika kwenye uwanja wa Old Traford alisema anajisikia furaha na hisia nyingi nzuri na zaidi akimtakia heri kocha Alex Ferguson ambaye alimsaidia kwa kiasi kikubwa kufikia malengo yake.

Ronaldo aliondoka Old Traford mwaka 2009 na kutua Real Madrid ambako ameondoka mwaka huu na kwenda Juventus. Pogba naye aliondoka Man United mwaka 2012 kwenda Juventus na kurejea 2016.

Man United na Juventus zimekutana mara 12 huku kila timu ikishinda mara 5 na zikitoka sare mara 2.
Ronaldo, Pogba kutengeneza historia UEFA Ronaldo, Pogba kutengeneza historia UEFA Reviewed by Zero Degree on 10/23/2018 09:35:00 AM Rating: 5

Powered by Blogger.