Loading...

Tetesi za soka barani Ulaya leo Jumatano Februari 27, 2019


Juventus haina mpango wa kumrudisha tena mshambuliaji wa kimataifa wa Argentina Gonzalo Higuain katika klabu hiyo mkataba wake wa bure utakapokamilika Chelsea. (Il Corriere di Torino)

Kipa wa Uhispani David de Gea, 28, anakabiliwa na hatari ya kushuka thamani nje ya Manchester United, licha ya klabu hiyo kuwa tayari kumpatia mkataba mpya wa euro £350,000 kwa wiki.

Roma wamekubaliana na uamuzi wa kuondoka kwa meneja wao wa kiufundi Monchi, huku Arsenal ikiongoza katika kampeini ya kumuajiri mhispania huyo wa miaka 50 msimu huu. (Evening Standard)

Ndugu wa mlinzi wa Chelsea Antonio Rudiger amesema mhispania Cesar Azpilicueta, 29, anastahili kuvuliwa kwa wadhifa wa unahodha na kupewa ndugu yake. (Mirror)

Ivan Rakitic, 30

Manchester United inamfuatilia kiungo wa kati wa Barcelona na Croatia Ivan Rakitic, 30.

Watford ni miongoni mwa vilabu vinavyomwania mlinzi wa Boavista Goncalo Cardoso, 18.

Kiungo huyo wa kimataifa wa Ufaransa anayechezea timu ya wachezaji wa chini ya miaka 21 amekuwa akifuatiliwa na Everton. (Mail)

Kipa wa Ajax na Cameroon Andre Onana, 22, yuko katika orodha ya kuwa kipa mpya wa Barcelona endapo Jasper Cillessen, 29, ataondoka klabu hiyo. (El Club de la Mitjanit)

West Brom wanamfuatilia mlinzi wa Crawley Town David Sesay, 20. (Sun)

Meneja wa Bradford Park Avenue Mark Bower ni anapigiwa upatu kuajiri na klabu ya Bradford City. (Telegraph & Argus)


Chanzo: BBC
Tetesi za soka barani Ulaya leo Jumatano Februari 27, 2019 Tetesi za soka barani Ulaya leo Jumatano Februari 27, 2019 Reviewed by Zero Degree on 2/27/2019 08:05:00 AM Rating: 5

Powered by Blogger.