Loading...

Tetesi za soka barani Ulaya leo Alhamisi Februari 28, 2019


Real Madrid inapania kumnunua beki wa kushoto wa Ajax muargentina Nicolas Tagliafico, 26, kuchukua nafasi itakayoachwa wazi na Marcelo.

Marcelo ambaye ni nyota wa kimataifa wa Brazil anajiandaa kujiunga na Juventus. (Tuttosport)

QPR huenda wakahamia uwanja wao mpya wenye uwezo wa kuhimili mashabiki 45,000 kama sehemu ya mradi wa maendeleo uliyogharimu euro milioni 425.

Manchester City wanamfuatilia mshambuliaji wa Benfica na Serbia Luka Jovic, ambaye anaichezea Eintracht Frankfurt kwa mkopo. (Mail)

Chelsea ni miongoni mwa vilabu vya ligi ya Primia vinavyomtafuta kiungo wa kati wa Croatia na Maritimo Josip Vukovic, 26. (Talksport)
Meneja wa Leicester Brendan Rodgers anataka kutumia euro milioni 40 kumjumuisha mshambuliaji wa Bournemouth na England Callum Wilson, 27 katika kikosi chake.

Mshambuliaji wa Ubelgiji Romelu Lukaku, 25, anapania kujiunga na Juventus endapo atalazimishwa kuondoka Manchester United.

Emiliano Martinez

Arsenal imemuita nyumbani kipa wake Emiliano Martinez ambaye amekuwa akichezea Reading kwa mkopo.

Emiliano anatarajiwa kuwa mlinda lango wa pili kwasababu hawana uwezo wa kumnunua kipa mwingine kuchukua nafasi ya Petr Cech anayeelekea kustaafu. (Sun)

Meneja wa Leeds United David Hockaday anasema alijaribu kumsajili mlinzi wa sasa wa Liverpool na Uholanzi Virgil van Dijk kutoka Celtic alipokuwa Elland Road, lakini ombi lake lilikatalliwa na mmiliki wa klbu hiyo Massimo Cellino. (Guardian)

Chelsea imewauliza mashabiki wake katika mtandao wa Twitter kupendekeza mchezaji ambaye wanataka asajiliwe na klabu hiyo licha ya marufuku ya usajili wa wachezaji inayowakabili. (Reuters)

Mshambuliaji wa Manchester United James Wilson, 23, anasema kuwa aliamua kuhamia Aberdeen kw amkopo msimu huu ili ''kujiuza''. (ESPN)

Chanzo: BBC
Tetesi za soka barani Ulaya leo Alhamisi Februari 28, 2019 Tetesi za soka barani Ulaya leo Alhamisi Februari 28, 2019 Reviewed by Zero Degree on 2/28/2019 08:20:00 AM Rating: 5

Powered by Blogger.