Loading...

Simba waonywa kwa Wawa


KOCHA Bora wa Ligi Kuu Tanzania Bara msimu wa 2017/18, Abdallah Mohamed ‘Bares’, amesema beki wa Simba, Pascal Wawa, hastahili kuendelea kuitumikia timu hiyo na badala yake uongozi unatakiwa kutafuta mlinzi bora zaidi yake.

Kwa mujibu wa taarifa ya Bingwa, Bares ambaye kwa sasa anakinoa kikosi cha JKT Tanzania, alisema Simba inatakiwa kufanya usajili kulingana na hadhi ya mashindano ya kimataifa watakayoshiriki mwakani.

“Binafsi kwa msimu ujao sioni kama Wawa anastahili kuendelea kuwapo Simba, kwani licha ya uzoefu wa kimataifa alionao lakini bado ana mapungufu mengi ambayo hayapaswi kuonekana katika kikosi hicho mwakani,” alisema kocha huyo.

“Ushauri wangu kwa benchi la ufundi la Simba na viongozi kwa ujumla watakapotaka kufanya usajili waanze na beki ambaye Wawa anacheza kisha wakaongeze nguvu mbele, kwani Emmanuel Okwi naye ameonekana kuchoka hivyo anahitaji wa kumsaidia.”
Simba waonywa kwa Wawa Simba waonywa kwa Wawa Reviewed by Zero Degree on 5/27/2019 11:35:00 AM Rating: 5

Powered by Blogger.