Chirwa akabidhiwa jukumu zito Azam FC
Mechi hiyo itapigwa nyumbani kwa Triangle nchini Zimbabwe huku wenyeji wakiwa na kumbukumbu ya ushindi wa bao 1-0 walioupata kwenye mechi ya kwanza hivyo Azam sasa wanahitaji ushindi wa mabao 2-0 ili watinge hatua inayofuata.
Ndayiragije alisema kuwa, amempa Chirwa jukumu la kufunga mabao kwa kuwa mchezaji huyo anaweza kufanya hivyo kutokana na uwezo wake mkubwa wa kupambana na mabeki.
“Nilizungumza na Chirwa na nikamwambia kuwa anatakiwa kufunga mabao mawili ya haraka zaidi ili tuweze kupata ushindi katika mchezo huu, kwa sababu nguvu na uwezo wa kupambana na mabeki wa Triangle anao, kama akiamua kujitolea zaidi basi hiyo itakuwa kazi ndogo sana kwake,” alisema Ndayiragije.
Chirwa akabidhiwa jukumu zito Azam FC
Reviewed by Zero Degree
on
9/29/2019 10:52:00 AM
Rating: