Barabara ya Jangwani yafungwa
BARABARA ya Jangwani jijini Dar es Salaam, imefungwa baada ya kujaa maji kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha nchini huku safari za mabasi yaendayo kasi kutoka Kimara kuelekea Kivukoni na Gerezani yakiishia Magomeni Mapipa.
Aidha, mabasi yanayofanya safari zake katika maeneo ya mjini, Muhimbili na Gerezani yataendelea kufanya safari zake pamoja na Kimara hadi Morocco kwani barabara zake hazina changamoto.
Maeneo mbalimbali mjini yameendelea kuwa na foleni kubwa kutokana magari mengi kutumia njia moja baada ya njia ya Jangwani kufungwa.
Maeneo mbalimbali mjini yameendelea kuwa na foleni kubwa kutokana magari mengi kutumia njia moja baada ya njia ya Jangwani kufungwa.
Barabara ya Jangwani yafungwa
Reviewed by Zero Degree
on
5/09/2024 12:05:00 PM
Rating:
Reviewed by Zero Degree
on
5/09/2024 12:05:00 PM
Rating:
