Loading...

Batshuayi amjibu Eden Hazard


Eden Hazard alimwambia mchezaji mwenzake, Michy Batshuayi abakie Stamford Bridge.

Mbelgiji huyo aliifungia Chelsea goli la ushindi kwenye Ligi ya Mabingwa dhidi ya klabu ya Atletico Madrid, ambapo Chelsea waliibuka na ushindi wa goli 2-1 ugenini.

Batshuayi ameweka wazi kwamba, Eden Hazard alimshauri abakie na mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya Uingereza.

“Ulikuwa ni ushauri unaofaa,” Batshuayi alisikika akiiambia ESPN.


“aliposema hivyo, alidhania kuna uwezekano wa kuwasili kwa mshambuliaji mwingine, lakini mwisho wa siku, tupo wawili tu katika nafasi moja.

“Ninataka kufanikiwa nikiwa ndani ya klabu hii na uhusiano wangu na Morata ni mzuri.

“Sitaki kuondoka mwezi Januari, kwa sababu tunaelekea kucheza michezo mingi na nina uhakika wa kupata nafasi ya kutosha.”
Batshuayi amjibu Eden Hazard Batshuayi amjibu Eden Hazard Reviewed by Zero Degree on 10/06/2017 01:26:00 PM Rating: 5

Powered by Blogger.