Loading...

Neymar: Huu ni "Unyama"

Wachezaji wa Brazil wakipata hewa ya oksijeni baada ya sare ya 0-0 dhidi ya Bolivia
Neymar amekosoa hali ya uwanja wa Estadio Hernando Siles ulioko mjini La Paz, nchini Bolivia kwa kusema kuwa ni "unyama" kuchezea katika mwinuko mkubwa kama ule.

Neymar, pia alilamikia mazingira ya uwanja na mpira uliotumika 
Kwa mujibuwa taarifa ya 'Sky Sports', wachezaji wa Brazili walihitaji huduma ya oksijine baada ya kumalizika kwa mchezo wa kufuzu kombe la dunia dhidi ya Bolivia ambayo iko futi 11,932 juu ya usawa wa bahari, mchezo ambao ulimalizika kwa sare ya bila kufungana.

Mshambuliaji huyo wa PSG ambaye ndiye mchezaji ghali zaidi duniani kwa sasa alisema "kila kitu kilikuwa vibaya" uwanjani na timu ilikuwa na furaha kwa kuweza kuondoka La Paz na pointi moja.



Neymar alipost kwenye ukurasa wake Instagram: "Sio ubinadamu kucheza katika hali ile, ....uwanja wa vile, mpira wenyewe na hali kadharika kwenye mwinuko kama ule ...kila kitu kilikuwa kibaya. Lakini pamoja na yote hayo, tulikuwa na furaha kwa kiwango tulichokionyesha."

Kocha mkuu wa timu ya taifa ya Brazil, Tite, ambaye ameifikisha Brazili katika nafasi ya kwanza kwenye kundi lao, alisema: "Lazima niawasifie wataalamu wetu kwa mipango yote iliyofanyika katika idara ya afya ambayo ilitoa msaada mkubwa kuwafanya wachezaji wasiteseke sana na mazingira yale.

"Kiwango kilikuwa cha kushangaza kwani, siku huwa ni vigumu sana kuchezea hapa. Ninafurahia kiwango kilichoonyeswa lakini sikupendezwa na matokeo ya mchezo."
Neymar: Huu ni "Unyama" Neymar: Huu ni "Unyama" Reviewed by Zero Degree on 10/06/2017 02:07:00 PM Rating: 5

Powered by Blogger.