Loading...

Rais Mugabe avuliwa cheo


Shirika la afya duniani WHO limefuta uteuzi wa rais wa Zimbabwe Robert Mugabe, kama balozi wa nia njema wa WHO.

"Nimesikiliza vizuri wale wote ambao wameelezea hisia zao," mkuu wa WHO Tedros Adhanom Ghebreyesus alisema katika taarifa.

Awali alikuwa ameisifu Zimbabwe kwa kujitolea kuboresha afya ya umma.

Lakini wakosoaji walisema kuwa mifumo ya afya nchini Zimbabwe iliporomoka chini ya utawala wa Mugabe wa miaka 30.

Wafanyakazi mara nyingi hukosa kulipwa na wakati mwingine
 dawa hukosekana huku Mugabe mwenyewe akisafiri nje ya nchi kupata matibabu.

Bw. Tedros alisema ameongea na serikali ya Zimbabwe na kuamua kuwa, suala la kumvua Mugabe wadhifa huo ni kwa manufaa ya WHO.

Alisema anasalia kujitolea kufanya kazi na chi zote na viongozi wake kujenga huduma bora za afya.

Uteuzi wa Bw. Mugabe ulipingwa vikali, 
kati ya wale ambao walikosoa uamuzi huo ni pamoja na Serikali ya Uingereza, waziri mkuu wa Canada na mashirika mengine kadha pamoja na watumiaji wa mitandao ya kijamii.

Kufuatia kukosolewa kutoka kwa mashirika ya haki za binadamu na kushangazwa kwa mataifa mengi wanachama, WHO haikuwa na lingine ila kufuata mpango wake wa kumvua Robert Mugabe wadhifa wa balozi wa nia njema.
Rais Mugabe avuliwa cheo Rais Mugabe avuliwa cheo Reviewed by Zero Degree on 10/23/2017 12:34:00 AM Rating: 5

Powered by Blogger.