Loading...

Mmoja afariki, wengine wafukiwa baada ya jengo la ghorofa 8 kuporomoka nchini Kenya


Mtu mmoja amefariki na watu kadhaa wamekwama katika jengo la orofa nane lililoporomoka katika eneo la Barani Malindi pwani ya Kenya Ijumaa alfajiri.


Inaarifiwa kwamba jengo hilo liliangukia majengo yaliokuwa karibu kikiwemo kituo cha mafuta pamoja na makaazi ya watu.

Haijulikani wazi nini kilichosababisha jengo hilo kuporomoka, licha ya kwamba mvua kubwa imekuwa ikinyesha kwa siku mbili mtawalia katika eneo hilo.

Mashirika ya kupambana na majanga kama vile shirika la msalaba mwekundu yanaendeleza operesheni ya uokozi, na idadi kamili ya watu waliokwama ndani ya kifusi haijulikani.

Kumekuwa na malalamiko kutoka kwa wakaazi kufuatia mafuriko ambayo yameshuhudiwa katika baadhi ya maeneo ya pwani.

Wakaazi wanazungumzia wasiwasi walio nao kufuatia mvua kubwa inayonyesha.

Katika eneo la mji wa Mombasa, barabara zilionekana kufurika maji , tatizo ambalo hushudiwa mara nyingi mvua kubwa inaponyesha kutokana na kuziba kwa mabomba ya kupitisha maji.

Hali ambayo pia imechangia kushuhudiwa kwa msongamano wa magari kwa wanaoingia na kutoka katika mji huo na viunga vyake.

Idara ya hali ya hewa nchini imetoa tahadhari ya mvua kubwa katika baadhi ya maeneo, tangu kaskazini mpaka kusini mwa Pwani.
Mmoja afariki, wengine wafukiwa baada ya jengo la ghorofa 8 kuporomoka nchini Kenya Mmoja afariki, wengine wafukiwa baada ya jengo la ghorofa 8 kuporomoka nchini Kenya Reviewed by Zero Degree on 10/26/2018 12:10:00 PM Rating: 5

Powered by Blogger.