Loading...

Serikali yakamilisha marekebisho ya kanuni za sheria ya Ngo's

Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto(Idara kuu ya Maendeleo ya jamii)Dk. John Jingu.
SERIKALI imekamilisha kuzifanyia marekebisho Kanuni tano za Sheria ya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali zitakazozitaka asasi za kiraia(AZAKI) kuweka wazi mambo mbalimbali ikiwemo vyanzo vya rasilimali zinazoendesha miradi yao.

Kauli hiyo ilitolewa leo jijini Dodoma na Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto(Idara kuu ya Maendeleo ya jamii)Dk. John Jingu, alipokuwa akifungua wiki ya asasi za kiraia kwa niaba ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.

Amesema kanuni hizo zimeshachapishwa kwenye gazeti la serikali namba 609, Oktoba 19 mwaka huu na zinalenga kuboresha utendaji kazi kwa asasi hizo.
Serikali yakamilisha marekebisho ya kanuni za sheria ya Ngo's Serikali yakamilisha marekebisho ya kanuni za sheria ya Ngo's Reviewed by Zero Degree on 10/22/2018 01:05:00 PM Rating: 5

Powered by Blogger.