Loading...

Kinachowaponza makocha wageni Azam hiki hapa


KOCHA aliyechukua mikoba ya kocha mkuu mkuu Hans Pluijm na Juma Mwambusi ambao walipigwa chini kutokana na mwenendo mbaya wa kikosi hicho kwenye ligi, Idd Cheche amesema makocha wa kigeni wengi hawatoi ushirikiano.

Cheche amesema kwa muda aliokaa ndani ya Azam FC amepata nafasi ya kuwatambua kwa ukaribu wachezaji kile wanachohitaji hali iliyompa nafasi kupata matokeo chanya kwenye mchezo wake wa kwanza.

"Unajua tatizo la wageni wengi ni kushindwa kutoa ushirikiano kwa wenyeji, wao wakija wanapenda kufanya maamuzi yao ambayo ni sahihi ila uzoefu wangu unanisaidia kupata matokeo.

"Nimekaa na wachezaji nikawajenga kisaikolojia na kuwapa maneno ya nguvu hali ambayo imewafanya wapambane na wapate matokeo chanya," amesema Cheche.

Jana Cheche aliongoza kikosi chake kikashinda mabao 3-0 mbele ya Rhino Rangers na kuifanya itinge hatua ya nane bora.
Kinachowaponza makocha wageni Azam hiki hapa Kinachowaponza makocha wageni Azam hiki hapa Reviewed by Zero Degree on 2/26/2019 09:05:00 AM Rating: 5

Powered by Blogger.