Loading...

JK ampa tano Lowassa kurejea CCM


Rais Mstaafu wa awamu ya nne, Dkt Jakaya Kikwete amempongeza Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa kwa uamuzi wake wa kurejea Chama cha Mapinduzi (CCM).

Lowassa alijiunga CHADEMA Julai 2015 baada ya jina lake kuenguliwa kwenye mchakato wa kutafuta mgombea wa urais ndani ya CCM.

“Karibu tena nyumbani, Hongera kwa uamuzi wa busara,” ameandika Dkt. Kikwete kwenye ukurasa wake wa mtandao wa Twitter.

Lowassa alitangaza hapo jana kurejea CCM katika ofisi ndogo za chama hicho zilizopo Lumumba Dar es Salaam na kupokelewa na Mwenyekiti wa CCM taifa, Rais John Magufuli.


JK ampa tano Lowassa kurejea CCM JK ampa tano Lowassa kurejea CCM Reviewed by Zero Degree on 3/02/2019 02:35:00 PM Rating: 5

Powered by Blogger.