Manara amuonya Mwinyi Zahera
Kupitia kipindi cha Sports HQ cha Radio EFM, Manara ameongea kimafumbo bila kutaja jina la Zahera akidai kuwa amesalia Dar es Salaam kuwapokea Vita na hajasafiri kwenda Iringa na timu yake.
Manara ameeleza kuwa Kocha huyo amekuwa akizunguka na Vita jijini Dar es Salaam bila kujua kama anapaswa kuwa na majukumu ya kuisaidia timu yake ambayo ina mechi na Lipuli Jumamosi hii huko Iringa.
Ofisa huyo amemuona Zahera kuwa makini na anachokifanya kwa sababu hii ni mechi ya kimataifa na kitaifa.
"Hii ni mechi ya kitaifa na ya kimataifa, tunaiwakilisha nchi, kuna kocha yeye kazi yake imekuwa ni kuzunguka na Vita tu na aliaga anaenda kwao Congo hata Iringa hajaenda.
"Hii ni mechi ambayo nchi inajua, Rais anajua, sasa ole wake aendelee kutuharibia mipango."
Manara amuonya Mwinyi Zahera
Reviewed by Zero Degree
on
3/15/2019 08:20:00 AM
Rating: