Dirisha la mikopo elimu ya juu kufunguliwa Julai Mosi
Mbali na kufungua dirisha hilo pia limebainisha bodi hiyo inawasiliana na Makao Makuu ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) ili kuweka utaratibu bora wa kuwawezesha wanafunzi wahitaji waliopo katika kambi za JKT kuwasilisha maombi kwa njia ya mtandao.
Taarifa ya Bodi hiyo iliyotolewa jana Jumanne Juni 25, 2019 na Mkurugenzi Mtendaji wake, Abdul-Razaq Badru ilisema kutokana na dirisha kukaribia kufunguliwa wanafunzi wanashauriwa kuhakikisha wanakamilisha nyaraka muhimu zinazohitajika na kutumia dakika 30 kukamilisha maombi hayo.
“Mwombaji anatakiwa kuambatanisha nakala ya cheti cha kuzaliwa cha mwombaji iliyothibitishwa na Rita au wakala wa Usajili wa matukio ya Kijamii Zanzibar (ZCSRA), nakala ya cheti cha kifo cha mzazi wa mwombaji iliyothibitishwa na Rita au ZCSRA.”
“Barua ya mganga mkuu wa Mkoa, wilaya au hospitali ya manispaa, wilaya, au jiji inayothibitisha ulemavu wa mwombaji au mzazi wake na barua kutoka taasisi iliyofadhili masomo ya sekondari au stashahada ya mwombaji mkopo,” amesema Badru
Amesema, “Mfumo wa uombaji mkopo kwa njia ya mtandao utakaofunguliwa haumlazimishi mwombaji kuwa na matokeo ya kidato cha sita bali atapaswa kuwa na namba ya mtihani wake wa kidato cha nne.”
Taarifa ya Bodi hiyo iliyotolewa jana Jumanne Juni 25, 2019 na Mkurugenzi Mtendaji wake, Abdul-Razaq Badru ilisema kutokana na dirisha kukaribia kufunguliwa wanafunzi wanashauriwa kuhakikisha wanakamilisha nyaraka muhimu zinazohitajika na kutumia dakika 30 kukamilisha maombi hayo.
“Mwombaji anatakiwa kuambatanisha nakala ya cheti cha kuzaliwa cha mwombaji iliyothibitishwa na Rita au wakala wa Usajili wa matukio ya Kijamii Zanzibar (ZCSRA), nakala ya cheti cha kifo cha mzazi wa mwombaji iliyothibitishwa na Rita au ZCSRA.”
“Barua ya mganga mkuu wa Mkoa, wilaya au hospitali ya manispaa, wilaya, au jiji inayothibitisha ulemavu wa mwombaji au mzazi wake na barua kutoka taasisi iliyofadhili masomo ya sekondari au stashahada ya mwombaji mkopo,” amesema Badru
Amesema, “Mfumo wa uombaji mkopo kwa njia ya mtandao utakaofunguliwa haumlazimishi mwombaji kuwa na matokeo ya kidato cha sita bali atapaswa kuwa na namba ya mtihani wake wa kidato cha nne.”
Dirisha la mikopo elimu ya juu kufunguliwa Julai Mosi
Reviewed by Zero Degree
on
6/26/2019 01:05:00 PM
Rating:
Reviewed by Zero Degree
on
6/26/2019 01:05:00 PM
Rating:
