Loading...

Polisi wakamata madini yakitoroshwa kuelekea Kenya


JESHI La polisi mpaka wa Namanga Wilaya ya Longido mkoani Arusha limekamata Madini ya aina mbalimbali zaidi ya kilo 36 yakitoroshwa kuelekea nchini Kenya.

Madini hayo yalikua yamepakiwa kwenye gari lilobeba mchele na kuwekwa katikati.

Polisi walitumia mbwa maalaum baadawa ukaguzi na kubaini madini hayo yakiwa yamefichwa katikati ya magunia ya mchele.

Madini yaliyokamatwa ni Tanzanite kg 24.2,Rubi kg 3.4, Green Ganet kg 3.0 na Madini mengine zaidi ya kg 5.9.

Mkuu wa Wilaya ya Longido, Frank Mwaisumbe, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kutoa tahadhari kwa watu wote wanaojihusisha na biashara za magendo.

Amesema watu wote wanaojihusisha na biashara za magendo kuacha mara moja kwani jeshi polisi lipo makini na endapo mtu atabainika na kukamatwa sheria itamshughulikia.

"Tuna jeshi makini na limeimarishwa tutawakamata wote mnaofanya Biashara za magendo" Amesema Mwaisumbe
Polisi wakamata madini yakitoroshwa kuelekea Kenya Polisi wakamata madini yakitoroshwa kuelekea Kenya Reviewed by Zero Degree on 6/26/2019 01:20:00 PM Rating: 5

Powered by Blogger.