Loading...

Msimamo wa Serikali kuhusu Watanzania kupewa saa 24 kuondoka Kenya



Waziri Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa amesema Serikali ya Kenya imemkana mbunge wa nchi hiyo, Charles Njagua Kanyi maarufu Jaguar aliyewapa saa 24 Watanzania waishio nchini humo kurejea makwao.

Akizungumza bungeni leo jioni Jumanne Juni 25, 2019 wakati akitoa kauli ya Serikali kuhusu kauli ya mbunge huyo kama alivyotakiwa kufanya hivyo na Spika Job Ndugai, Majaliwa amesema Serikali ya Kenya tayari imemtaka aeleze alitoa kauli hiyo akiwa analenga nini.

Kabla ya Ndugai kumpa nafasi Majaliwa kutoa maelezo ya Serikali, aliwapa nafasi wabunge kutoa maoni yao ikiwa ni baada ya kudai haoni umuhimu wa Serikali kumjibu mbunge mmoja.

Miongoni mwa waliotoa maoni yao ni Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe.

Video inayosambaa katika mitandao mbalimbali ya kijamii inamuonyesha Jaguar ambaye ni mwanamuziki maarufu ndani na nje ya Kenya, akitoa maagizo hayo huku akiwa amezungukwa na umati wa wananchi waliomshangilia na kusindikiza kila eneo alilopita.

Kauli ya Jaguar iliombewa mwongozo bungeni leo mchana na mbunge wa Rufiji (CCM), Mohammed Mchengerwa aliyetaka kujua kauli ya Serikali, Ndugai kumtaka Majaliwa kutoa kauli ya Serikali.
Msimamo wa Serikali kuhusu Watanzania kupewa saa 24 kuondoka Kenya Msimamo wa Serikali kuhusu Watanzania kupewa saa 24 kuondoka Kenya Reviewed by Zero Degree on 6/26/2019 09:51:00 AM Rating: 5

Powered by Blogger.