Loading...

Tetesi za soka barani Ulaya Jumatano Tarehe 8 Mei, 2024

Meneja wa klabu ya Manchester United, Erik ten Hag

Manchester United hawana nia ya kumfukuza meneja Erik ten Hag kabla ya fainali ya Kombe la FA, mnamo Mei 25.

Kocha wa klabu ya Bayern Munich Thomas Tuchel ana nia ya kuwa meneja wa Manchester United iwapo klabu hiyo itaamua kumfukuza Ten Hag. (Telegraph)

The Blues pia wamemtambua mlinda lango wa Everton Muingereza Jordan Pickford, 30, kama wanayemlenga majira ya joto.

Hata hivyo, Mholanzi Ten Hag atafutwa kazi mwishoni mwa msimu huu. (Football Insider)

Tuchel ndiye mgombea anayeongoza kuchukua mikoba Old Trafford, lakini kocha wa Sporting Lisbon Ruben Amorim na meneja wa zamani wa Chelsea Graham Potter pia wako kwenye kinyang'anyiro. (Habari)

Meneja wa zamani wa klabu ya Manchester United, Jose Mourinho angependa kurejea kwa kipindi cha pili lakini klabu hiyo haitaki kumteua tena Mreno huyo mwenye umri wa miaka 61, ambaye alitimuliwa na klabu ya AS Roma mwezi Januari. (Manchester Evening News)

Klabu ya Crystal Palace wako tayari kumuuza mlinzi wa Uingereza Marc Guehi, 23, badala ya kumtoa winga kutoka Ufaransa Michael Olise, 22, au winga wa Uingereza Eberechi Eze, 25, msimu huu. (Givemesport)

West Ham wameanza mazungumzo ya kumsajili winga wa Corinthians, 19, raia wa Brazil, Wesley Gassova, ambaye pia analengwa na Liverpool. (Standard)

Chelsea inatafuta mnunuzi wa mshambuliaji wa Albania Armando Broja kufuatia kipindi cha mkopo cha mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 22 na Fulham. (Fabrizio Romano)

Chelsea wako kwenye mazungumzo ya kumsajili winga Estevao Willian,17 kutoka Palmeiras. (Usajili unahitajika)


Newcastle na Inter Milan wameingia kwenye kinyang'anyiro cha kumsajili beki wa Barcelona na Ufaransa Jules Kounde , 25 , ambaye pia amewavutia Chelsea , Manchester United na Paris St-Germain. (Mundo Deportivo)

Mshambulizi wa Roma na England Tammy Abraham yuko tayari kurejea kwenye Ligi ya Premia, huku West Ham ikiwa moja ya timu zinazomfuatilia mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26. (HITC)

Barcelona wanafikiria kumrejesha meneja wa Paris St-Germain Luis Enrique kwenye klabu ili kurithi mikoba ya Xavi mwaka wa 2025. (Sport)
Tetesi za soka barani Ulaya Jumatano Tarehe 8 Mei, 2024 Tetesi za soka barani Ulaya Jumatano Tarehe 8 Mei, 2024 Reviewed by Zero Degree on 5/08/2024 09:06:00 AM Rating: 5

Powered by Blogger.