Loading...

Lowassa apinga matokeo ya uchaguzi TZ

Mgombea wa urais kupitia tiketi ya chama cha CHADEMA Edward LOwassa amesema kuwa hatokubali matokeo ya uchaguzi wa urais yanayoendelea kutolewa na tume ya uchaguzi nchini Tanzania NEC.

Amesema kuwa ana ushahidi wa kutosha kwamba kuna udanganyifu uliofanyika.
Amesema kuwa kura za chama hicho zimepunguzwa katika vituo vingi vya kupigia kura.
Wanadai kwamba kura zilizohesabiwa katika maeneo tofauti haziambatani na matokeo yaliotolewa.
Lowassa ameongezea kwamba maeneo yote ambayo walipata ushindi yamecheleweshwa huku kukamatwa kwa maajenti wa chama hicho akidai kuwa ni ishara za kutaka kuiba kura.
Credits: BBC
Lowassa apinga matokeo ya uchaguzi TZ Lowassa apinga matokeo ya uchaguzi TZ Reviewed by Zero Degree on 10/28/2015 01:55:00 PM Rating: 5

Powered by Blogger.