Loading...

Watu 11 wamefariki dunia na wengine 29 kujeruhiwa baada ya basi la abiria kugongana na lori wilayani Muheza.


Tanga. Watu 11 wamefariki dunia leo huku wengine 29 wamejeruhiwa baada ya Basi la Simba Mtoto kugongana uso kwa uso na lori katika kijiji cha Pangamlima wiliyani Muheza.

Kamanda wa polisi Mkoani Tanga, Mihayo Msikhela amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kuongeza kuwa Basi la Simba Mtoto lilikuwa linatokea Tanga kuelekea jijini Dar es salaam.

Kamanda Mihayo ameeleza kuwa ajali hiyo imetokea mapema leo baada ya dereva wa lori kuhama njia na kukutana uso kwa uso na basi hilo.

Pia kamanda Mihayo amesema kuwa, kati ya watu 11 waliopoteza maisha ni pomoja na madereva wa magari hayo mawili.

Kamanda Mihayo ameongeza kuwa majeruhi wamepelekwa katika hospitali ya wilaya ya Muheza huku jitihada zikifanyika kuwapeleka abiria watano ambao hali zao ni mbaya katika hospitali ya rufaa ya KCMC mjini Moshi mkoani Kilimanjaro.

Credits: Mwananchi





ZeroDegree.
Watu 11 wamefariki dunia na wengine 29 kujeruhiwa baada ya basi la abiria kugongana na lori wilayani Muheza. Watu 11 wamefariki dunia na wengine 29 kujeruhiwa baada ya basi la abiria kugongana na lori wilayani Muheza. Reviewed by Zero Degree on 2/11/2016 04:36:00 PM Rating: 5

Powered by Blogger.