Loading...

Taarifa ya polisi Dar baada ya kumalizika kwa zoezi la uhakiki wa silaha.

Polisi kanda maalum ya Dar es salaam leo July 22 2016 wametoa majumuisho ya zoezi la uhakiki wa silaha
mkoa wa Dar es salaam lililofanyika kwa miezi mitatu, zoezi hilo lilianza March 1, 2016 na limemalizika June 30, 2016.

Kamishna wa polisi kanda maalumu ya Dar es salaam, Simon Sirro ametoa taarifa hiyo mbele ya wandishi wa habari na kusema idadi ya watu waliojitokeza kuhakiki silaha kwa wilaya zote tatu ni 11,602 na jumla ya silaha 14107 zilihakikiwa.

Jumla ya silaha 66 zilisalimishwa kutokana sababu mbalimbali ikiwamo mmiliki wa silaha kuwa na umri mkubwa na kushindwa kumudu silaha. Zoezi la uhakiki wa silaha limeiingizia Serikali mapato kiasi cha Mil 198.8.


Itazame taarifa hiyo hapa.


Credits: MillardAyo
ZeroDegree.
Taarifa ya polisi Dar baada ya kumalizika kwa zoezi la uhakiki wa silaha. Taarifa ya polisi Dar baada ya kumalizika kwa zoezi la uhakiki wa silaha. Reviewed by Zero Degree on 7/22/2016 07:36:00 PM Rating: 5

Powered by Blogger.