Loading...

SIMBA yaitisha Mkutano Mkuu utakaofanyika Tar 11 Desemba.

UONGOZI wa klabu ya Simba umeitisha mkutano wa wanachama wa dharura utakaofanyika Desemba 11.

Mkutano huo umeitishwa baada ya kikao cha Kamati ya Utendaji wa klabu hiyo iliyokaa juzi.

Kwa mujibu wa msemaji wa Simba, Haji Manara, mkutano huo utafanyika kwenye ukumbi wa Bwalo la Maofisa wa Polisi Oysterbay jijini Dar es Salaam.

Alisema Kamati ya Utendaji imetoa baraka zake kupitia ibara ya 22 ya Katiba ya Simba.

“Mkutano huo utakuwa ni mwendelezo wa mkutano wa kawaida uliofanyika Julai 31, 2016,” alisema Manara.

Hata hivyo, taarifa hiyo haijaeleza ajenda za mkutano huo, lakini inadaiwa kuwa huenda ukahusu kuboresha suala la uongozi wa Simba na kuingia katika suala la uwekezaji.

ZeroDegree.
SIMBA yaitisha Mkutano Mkuu utakaofanyika Tar 11 Desemba. SIMBA yaitisha Mkutano Mkuu utakaofanyika Tar 11 Desemba. Reviewed by Zero Degree on 11/22/2016 11:04:00 AM Rating: 5

Powered by Blogger.