Loading...

Aliyekuwa kiungo wa zamani wa Misri Mohamed Aboutrika ahusishwa na ugaidi

Mamlaka za usalama za Egypt zimemweka mchezaji wa zamani wa soka wa timu ya taifa ya Egypt, Mohamed Aboutrika katika listi ya magaidi baada ya kuhusishwa na kikundi cha waislam wa Brotherhood, amesema mwanasheria wa mchezaji huyo.

Aboutrika anashutumiwa kuwasaidia kifedha kikundi cha Brotherhood, kikundi ambacho mamlaka za Misri kimewaeka kwenye kundi la magaidi.

Mnamo mwaka 2012, alimpigia kampeni ya urais Mohamed Morsi, ambaye ni mwanachama wa Brotherhood.

Jambo hilo lilipelekea kuwagawa mashabiki wa mchezaji bora wa mwaka wa BBC wa mwaka 2008.

Kwa sheria za Misri, mtu yoyote anayewekwa kwenye listi ya ugaidi, hufungiwa kusafiri na passport yake pamoja na mali zake hushikiliwa.

Mwanasheria wa Aboutrika, Mohamed Osman, alisema mteja wake hajatiwa hatiani wala hajapewa taarifa rasmi juu ya mashtaka wanayomtuhumi nayo. Pia ameahidi kukata rufaa juu ya tuhuma hizo kwa mteja wake.

Kiungo huyo wa zamani wa Al-Ahly na timu ya taifa ya Misri, alikuwa kipenzi cha wananchi wa Misri na walifikia hatua ya kumpa majina ya The Prince of Hearts, The Magician na The Saint wakati akicheza soka, lakini uamuzi wake wa kumsapoti Mohammed Morsi, ambaye alikaa madarakani kwa mwaka mmoja tu, uliwagawa mashabiki zake.

Mwaka 2015, mali zake nyingi ziliwekwa kizuiani, hisa zake kwenye makampuni tofauti zilishikiliwa na mamlaka za usalama za nchi hiyo.

ZeroDegree.
Aliyekuwa kiungo wa zamani wa Misri Mohamed Aboutrika ahusishwa na ugaidi Aliyekuwa kiungo wa zamani wa Misri Mohamed Aboutrika ahusishwa na ugaidi Reviewed by Zero Degree on 1/18/2017 06:29:00 PM Rating: 5

Powered by Blogger.