Loading...

Askofu aapishwa kuwa kiongozi mkuu wa tume ya kupambana na Rushwa Kenya

Askofu Wabukala anatajaria kufaulu katika utendaji mahali ambapo wengi wameshindwa
Mkuu mpya wa tume ya kupambana na rushwa nchini Kenya ameapishwa rasmi mjini Nairobi.

Askofu Eliud Wabukala ambaye alikuwa mkuu wa kanisa la kianglikana, alisema anachukua wajibu huo wakati ufisadi unaonekana kukithiri nchini Kenya.

Pia alisema kuwa atahitaji ushirikiano wa mashirika mengine ya serikali kusiaia katika jitidsja za kuamana na ufoisadi. Amenya kwua watu ni alzima wacha kuiba pesa "kuanzia leo".

Mkuu wa sheria nchini Kenya Githu Muigai alimpongeza bwana Wabukala akisema kuwa hakuna mikono bora wa kupigana na vita hivyo ila mikono ya Mungu.

Jitihada za wakuu wa awali wa tume ya kupambana na rushwa zilitatizwa baada ya wao wenyewe kulaumiwa kwa kuhusika kwenye ufisadi.

Source: BBC Swahili
ZeroDegree.
Askofu aapishwa kuwa kiongozi mkuu wa tume ya kupambana na Rushwa Kenya Askofu aapishwa kuwa kiongozi mkuu wa tume ya kupambana na Rushwa Kenya Reviewed by Zero Degree on 1/23/2017 05:27:00 PM Rating: 5

Powered by Blogger.