Loading...

Scholes atabili nafasi watakayomaliza nayo Man U katika Ligi mwishoni mwa msimu huu

MANCHESTER United itamaliza msimu huu wa Ligi Kuu England ikiwa nafasi ya tatu, kwa mujibu wa kiungo wa zamani wa timu hiyo, Paul Scholes.

Scholes alisema sababu kubwa ni umaliziaji wao mbaya, la wangeweza kuwa kwenye vita ya kushindania ubingwa wa ligi msimu huu.

Kikosi hicho kinachonolewa na Jose Mourinho, ambacho kipo kwenye fomu nzuri kwa sasa kimecheza mechi 16 bila ya kupoteza, lakini bado kimebaki kwenye nafasi ya sita, pointi mbili tu nyuma ya timu inayoshika nafasi ya nne.

Scholes alisema ni kwamba Man United wanapaswa kubadili na kurekebisha udhaifu wao kwenye umaliziaji.

“Ni mabadiliko makubwa sana kutoka kile tulichokuwa tukikiona miaka ya karibuni. Miezi miwili au mitatu hawakuwa vizuri, lakini sasa wamechenji kila kitu. Wanacheza staili ambayo mashabiki wanaburudika. Tatizo lao bado wapo nafasi ya sita, kwa kuwa na kiwango kizuri hiki kuendelea kuwa hapo, inatia shaka,” alisema.

“Wanacheza soka nzuri sana katika timu hizo sita sambamba na Chelsea na nawaona wakimaliza nafasi ya pili au tatu. Hasa hasa ya tatu,” alisema.

Scholes atabili nafasi watakayomaliza nayo Man U katika Ligi mwishoni mwa msimu huu Scholes atabili nafasi watakayomaliza nayo Man U katika Ligi mwishoni mwa msimu huu Reviewed by Zero Degree on 2/18/2017 06:21:00 PM Rating: 5

Powered by Blogger.