Loading...

Simu aliyokuwa anatumia Adolf Hitler kuuzwa mnadani nchini Marekani

Simu iliokuwa ikitumiwa na kiongozi wa Nazi Adolf Hitler kupigwa mnada Marekani
Simu iliyokuwa ikitumiwa na Adolf Hitler wakati wa vita vikuu vya pili vya Dunia itapigwa mnada nchini Marekani mwisho mwa juma hili.

Simu hiyo nyekundu iliyo na chapa ya jina la kiongozi huyo wa Wanazi, ilipatikana katika ngome ya Hitler jijini Berlin mwaka 1945.

Wanajeshi wa Urusi walimpa mwanajeshi wa Uingereza, Brigedia Sir Ralph Rayner, kama kito cha kumbukumbu, muda mfupi baada ya Ujerumani kukubali kushindwa katika vita hivyo.

Simu ya Adolf Hitler
Kampuni hiyo ya mnada iliyoko Maryland, ilisema kuwa shughuli za mnada zitaanza kwa bei ya Dola 100,000.

Source: BBC Swahili
Simu aliyokuwa anatumia Adolf Hitler kuuzwa mnadani nchini Marekani Simu aliyokuwa anatumia Adolf Hitler kuuzwa mnadani nchini Marekani Reviewed by Zero Degree on 2/18/2017 05:05:00 PM Rating: 5

Powered by Blogger.