Loading...

Haji Manara: Hans Pope amefuta uamuzi wake wa kujiuzulu uongozi Simba SC

Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba, Zacharia Hanspope amerudi kundini Simba baada ya kufuta uamuzi wake wa kujiuzulu.

Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano wa Simba, Haji Manara amethibitisha suala hilo na kusema Hanspope amerudi kundini baada ya kujiuzulu kutokana na sakata liloendelea ndani ya Simba.

Baada ya kuripotiwa taarifa za kujiuzulu kwa Hans Pope Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili wa Simba, leo Jumatatu May 15, 2017 ripoti mpya kutoka kwa Afisa Habari wa club hiyo Haji Manara, ambaye Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano wa Simba, Haji Manara amethibitisha suala hilo na kuandika kwenye ukurasa wake wa Instagram kwamba Hanspope amefuta uamuzi wake.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Haji Manara ameandika: Rasmi Hanspope arejea kundini, afuta uamuzi wake wa kujiuzulu, na ndio maana fans wetu nawaomba mtulie, hakuna kitakachoharibika, ni upepo mbaya ulipita na sasa umetulia, Karibu tena kamanda Pope – Manara.
Haji Manara: Hans Pope amefuta uamuzi wake wa kujiuzulu uongozi Simba SC Haji Manara: Hans Pope amefuta uamuzi wake wa kujiuzulu uongozi Simba SC Reviewed by Zero Degree on 5/15/2017 12:33:00 PM Rating: 5

Powered by Blogger.