Loading...

Watoto wawili wamefariki dunia na wengine wawili kunusurika katika ajali ya moto jijini Mwanza

Picha ya Mtandao
Watoto wawili wa kiume mmoja na wa kike mmoja wakazi wa mtaa wa Kigoto, wilayani Ilemela Jijini Mwanza wamefariki dunia na wengine wawili kunusurika kifo katika ajali ya moto iliyosababishwa na mshumaa kushika kwenye kochi huku mama wa watoto hao akijeruhiwa na moto huo wakati akiwaokoa watoto wake.

Wakizungumza katika tukio majirani wa familia hiyo wamesema kuwa moto huo umeanza kuwaka majira ya saa nne usiku na kwamba wamefanya jitihada za kuwaokoa watoto hao lakini kutokana na moto kuwaka kwa kasi wameshindwa kuwaokoa watoto wawili

Nae baba mzazi wa watoto hao, Said Daudi amesema kuwa wakati moto huo unawaka katika nyumba yake hakuwepo nyumbani hivyo alikuwepo mama yao na alikuwa nje huku watoto wakiwa ndani ndipo mshumaa ulishika kwenye kochi na kusababisha madhara hayo

Kwa uapnde wa kaimu mwenyekiti wa mtaa huo, Zakayo Yusuph amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuwomba wananchi kuwa makini na matumizi ya mishumaa.

Katika hatua nyingine mwenyekiti huyo amewataka wananchi kuzingatia matumizi ya mishumaa kwa lengo la kuepuka na majanga ya moto pindi wanapotumia.
Watoto wawili wamefariki dunia na wengine wawili kunusurika katika ajali ya moto jijini Mwanza Watoto wawili wamefariki dunia na wengine wawili kunusurika katika ajali ya moto jijini Mwanza Reviewed by Zero Degree on 6/23/2017 02:00:00 PM Rating: 5

Powered by Blogger.