Loading...

Lampard katika mazungumzo kuwania nafasi ya meneja iliyoachwa wazi na Michael Appleton


Nyota wa zamani wa Chelsea, Frank Lampard inaonekana hivi karibuni amefaanya mazungumzo na Oxford United kuhusiana na nafasi ya Meneja ambayo iko wazi hadi hivi sasa.

Sky Sports walitoa ripoti hii Twitter
Michael Appleton
Kwa mujibu wa ripoti mbali mbali, Frank Lampard tayari amefanya mazunguzo na Oxford United juu ya nafasi ya meneja iliyoachwa wazi kufuatia kuondoka kwa Michael Appleton aliyeelekea Leicester City hivi karibuni.

Kwa uamuzi wa Appleton kutimukia Leicester kufanya kazi na Craig Shakespeare akiwa kama msaidizi wake, Oxford United wako kwenye msako wa atakayerithi nafasi yake, na hivi karibuni Lampard ndiye ameonekana kuwa na nafasi kubwa ya kupewa kazi hiyo.

'Sky Sports' wameripoti kwamba, kiungo huyo wa zamani wa Chelsea amefanya vikao kadhaa na klabu hiyo inayoshiriki Ligi ya daraja la kwanza Uingereza ambayo inaonekana kuwa na nia thabiti ya kumpa kazi yake ya kwanza kama meneja.

Hata hivyo, inaonekana kuna idadi kubwa ya watu wengine wanaowania nafasi hiyo ambao wanategemewa kufanya mazungumzo na klabu hiyo siku za mbeleni, akiwemo Pep Clotet, ambaye amefanya kazi kama msaidizi wa Garry Monk wakiwa na klabu ya Swansea na Leeds.
Lampard katika mazungumzo kuwania nafasi ya meneja iliyoachwa wazi na Michael Appleton Lampard katika mazungumzo kuwania nafasi ya meneja iliyoachwa wazi na Michael Appleton Reviewed by Zero Degree on 7/01/2017 10:46:00 AM Rating: 5

Powered by Blogger.