Majibu ya Zidane juu ya mdaharo wa nani atatwaa tuzo ya Ballon d'Or
Watu wengi walitegemea kocha wa Real Madrid, Mfaransa Zinedine Zidane naye angeonesha upande anaoupa asilimia kubwa katika kinyang'anyiro hicho, lakini imekuwa tofauti.
Zidane amedhihirisha kwamba hana mpango wa kumpa ushindi mchezaji yeyote anayewania tuzo hiyo.
Kwa mujibu wa taarifa ya Daily Mirror, Mfaransa huyo alisema: "Siko tayari kuwa upande wowote katika mdaharo huu".
"Tuzo ya Ballon d'Or, ni kitu kingine kabisa, kitu ambacho kinawahitaji watu kupiga kula."
Majibu ya Zidane juu ya mdaharo wa nani atatwaa tuzo ya Ballon d'Or
Reviewed by Zero Degree
on
10/17/2017 06:47:00 PM
Rating: