Loading...

Msanii mkongwe wa muziki wa Jazz Afrika Kusini, Hugh Masekela afariki dunia

Hugh Masekela
Tasnia ya muziki nchini Afrika Kusini imekumbwa na majonzi kwa kumpoteza Hugh Masekela ambaye alikuwa mpiga trumpeter mkongwe nchini humo.

Masekela amefariki Jumanne hii akiwa na umri wa miaka 78 kwa maradhi ya saratani.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na familia yake imesema, “Baada ya vita vya muda mrefu na ujasiri na saratani ya kinga, amefariki kwa amani huko Johannesburg, Afrika Kusini, akizungukwa na familia yake.”

Naye Rais wa nchi hiyo Jacob Zuma ametuma salamu zake za rambi rambi kwa familia ya marehemu kwa kusema, “Taifa linaomboleza kipaji kimoja kinachojulikana zaidi … Ni kupotea kabisa kwa sekta ya muziki kwa nchi nzima. Mchango wake katika mapambano ya ukombozi kamwe hauwezi kusahaulika.”

Hugh Masekela enzi za uhai wake
“Tunataka kufikisha matumaini yetu ya moyo kwa familia yake na wenzake katika ushirika wa wasanii na utamaduni kwa ujumla. Na nafsi yake ipumzike kwa amani,” ameongeza.
Msanii mkongwe wa muziki wa Jazz Afrika Kusini, Hugh Masekela afariki dunia Msanii mkongwe wa muziki wa Jazz Afrika Kusini, Hugh Masekela afariki dunia Reviewed by Zero Degree on 1/23/2018 06:31:00 PM Rating: 5

Powered by Blogger.