Loading...

Jezi ya timu ya taifa ya Nigeria yazua gumzo kuelekea Kombe la Dunia Urusi


Nigeria huenda sio wanaopigiwa upatu kushinda kombe la dunia lakini wanaonekana kupata mashabiki wengi kupitia jezi yao mpya.

Mashabiki milioni 3 tayari wameagiza tisheti kama hizo kulingana na shikisho la soka la Nigeria na wanunuzi walipanga foleni nje ya duka la kampuni ya jezi ya Nike mjini London siku ya Ijumaa ili kujaribu kununua nguo hizo.

Tisheti hizo zilizokuwa zinauzwa kwa bei ya £64.95, ziliuzwa katika tovuti ya kampuni ya Nike muda mfupi baada ya kutolewa.

Kiungo wa kati wa Arsenal Alex Iwobi ni miongoni mwa waliouza jezi hizo ambazo zilizinduliwa kwa mara ya kwanza mnamo mwezi Februari , pamoja na mchezaji wa Leicester Wilfried Ndidi, ambaye alivaa kofia na jaketi katika picha za kampeni ya kuziuza jezi hizo.

Alex Iwobi na Wilfried Ndidi ni miongoni mwa wachezaji wa ligi ya Uingereza waliokuwa wanamitindo wa kuuza nguo hizo mpya
Nigeria inatarajiwa kuvaa jezi hizo mpya wakati itakapokabiliana na Uingereza katika mechi ya kirafiki ya kombe la dunia katika uwanja wa Wembley Jumamosi Usiku.
Jezi ya timu ya taifa ya Nigeria yazua gumzo kuelekea Kombe la Dunia Urusi Jezi ya timu ya taifa ya Nigeria yazua gumzo kuelekea Kombe la Dunia Urusi Reviewed by Zero Degree on 6/02/2018 04:05:00 PM Rating: 5

Powered by Blogger.