Loading...

Simba kushusha kiboko ya Mkude


MBABANE Swallows wamethibi­tisha nia ya Simba kumsainisha kiungo wao tegemeo, Njabulo Ndlo­vu kabla ya dirisha dogo kufungwa Jumamosi.

Simba inataka kumsajili mchezaji huyo ili kuima­risha safu ya kiungo kwavile Kocha Patrick Aussems amemuelewa mavitu yake.

Ingawa Swallows wamethibitisha kupitia ukurasa wao wa Facebook jana Juma­tano lakini habari kutoka ndani ya Simba zinasema kwamba ni chaguo la Aussems.

Habari zinasema kwamba Aussems ame­vutiwa na uchezaji wa Nd­lovu ambaye anadhani ni mchezaji sahihi wa kumpa changamoto Jonas Mkude kwenye kiungo cha Simba.

Simba ingawa wana mechi ngumu dhidi ya Nka­na Jumamosi jijini Kitwe, Zambia lakini vigogo wen­gine wanaendelea na harakati za kumaliza dili la Ndlovu kwani usajili utamalizika Jumamosi hiyohi­yo wakiwa ugenini kabla dirisha hali­jafungwa
Simba kushusha kiboko ya Mkude Simba kushusha kiboko ya Mkude Reviewed by Zero Degree on 12/13/2018 05:05:00 PM Rating: 5

Powered by Blogger.