Breaking News: Mo Dewji apatikana
Akitoa taarifa hizo kuptia mtandao wa Twitter unaomilikiwa na Kampuni yake ya Mohamed Enterprises Ltd, Mo ameandika: “Namshukuru Mwenyezi Mungu nimerudi salama nyumbani. Nawashukuru Watanzania wenzangu na watu wote kote duniani kwa dua na sala zao. Nashukuru mamlaka zote, ikiwemo Jeshi la Polisi, zilizofanya kazi ya kuhakikisha narudi salama.” — Mohammed Dewji na , taarifa ambayo aliipost Saa 9:15 alfajiri, saa za Tanzania.
Aidha, Waziri wa Mazingira, Mhe. Januari Makamba, nae kupitia mtandao wake wa Twitter, amethibitisha kupatikana kwa Mo na kusema kuwa Mfanyabiashara huyo alitupwa maeneo ya Gymkhana huku akiwa na alama za kufungwa kamba mikononi.
“Nimemuona na kuongea kwa kirefu na Mohammed Dewji. Ni mzima wa afya isipokuwa ana alama za kufungwa kamba mikononi na miguuni. Mnamo saa nane usiku, watekaji waliamua kumtupa kwenye maeneo ya viwanja vya Gymkana. Naamini Polisi watatoa taarifa za ziada kuhusu kilichojiri.,” ameandika Makamba.
Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa amethibitisha kupatikana kwa Mo Dewji.
Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa amethibitisha kupatikana kwa Mo Dewji.
Breaking News: Mo Dewji apatikana
Reviewed by Zero Degree
on
10/20/2018 07:50:00 AM
Rating: