Loading...

Vikosi vinavyotarajiwa kuanza leo Yanga Vs Simba


Leo Jumamosi, Yanga ikitarajiwa kupambana na Simba, tayari kocha wa timu hiyo, Mwinyi Zahera ameshapata kikosi cha kwanza kitakachoanza katika mchezo huo.
Yanga ambayo inaongoza ligi hiyo ikiwa na pointi 58, itakuwa mwenyeji wa mchezo huo utakaochezwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Kikosi cha Yanga ambacho kimepiga kambi mkoani hapa tangu Jumatatu ya wiki hii, kime­kuwa kikifanya mazoezi kwenye Uwanja wa Chuo cha Biblia uliopo Bigwa.
Katika mazoezi ya jana asub­uhi, Zahera raia wa DR Congo, alionekana kuwa makini na kikosi ambacho kinaaminika ndicho kitaanza katika mchezo huo wa kesho.

Kikosi hicho kilikuwa kinaun­dwa na Ramadhan Kabwili, Paul Godfrey ‘Boxer’, Gadiel Michael, Andrew Vincent ‘Dante’, Kelvin Yondani, Abdallah Shaibu ‘Ninja’, Mrisho Ngassa, Feisal Salum ‘Fei Toto’, Heritier Makambo, Papy Tshishimbi na Ibrahim Ajibu.

Aussems kushangaza wengi:

KOCHA Mkuu wa Simba, Patrick Aussems, leo Jumamosi anaweza kuwashangaza wengi kwa namna ambavyo atapanga kikosi chake cha kwanza kuna uwezekano mshambuliaji tegemeo timu hiyo, Emmanuel Okwi, akaanzia benchi.

Licha ya Aussems kusema kutakuwa na mabadiliko kwenye kikosi chake cha leo, lakini kuna uwezekano mkubwa wa kikosi hicho kikawa hivi; Aishi Manula, Zana Coulibaly, Mohammed Hussein ‘Tshabalala’, Juuko Murshid, Pascal Wawa, James Kotei, Clatous Chama, Jonas Mkude, John Bocco, Meddie Kagere na Hassan Dilunga.
Vikosi vinavyotarajiwa kuanza leo Yanga Vs Simba Vikosi vinavyotarajiwa kuanza leo Yanga Vs Simba Reviewed by Zero Degree on 2/16/2019 08:40:00 AM Rating: 5

Powered by Blogger.