DPP afuta kesi ya mauaji iliyokuwa ikimkabili mfanyabishara wa Tabora kwa madai alibambikiwa
Hatua hiyo inafikiwa baada ya mmoja wa watuhumiwa Mussa Adam Sadick kuandika barua ya wazi na kuomba msaada kwa rais John Pombe Magufuli kwenye moja ya chombo cha habari kwa madai ya kukamatwa na polisi bila kosa na kufikishwa mahakamani mnamo tarehe 6/5/2018 na kusomewa shtaka la mauaji na kisha kuunganishwa na Edward Nduli ambaye alikuwa hamjui katika shtaka hilo
Barua hiyo ilisomwa na rais Magufuli ambaye aliagiza ofisi ya DPP kufuatilia kesi hiyo na ndipo ilipobaini malalamiko hayo ni ya kweli na mnamo tarehe 8/3/2019 iliwafutia washtakiwa wote mashtaka na mahakama imewaachia huru.
Aidha DPP Mganga amesema kufuatia tukio hilo rais John Pombe Magufuli ameagiza hatu kali za kisheria zichukuliwe kwa waliohusika ili kukomesha tabia hizo zinazoichafua serikali kwa wananchi wake na dunia nzima
Chanzo: ITV
Barua hiyo ilisomwa na rais Magufuli ambaye aliagiza ofisi ya DPP kufuatilia kesi hiyo na ndipo ilipobaini malalamiko hayo ni ya kweli na mnamo tarehe 8/3/2019 iliwafutia washtakiwa wote mashtaka na mahakama imewaachia huru.
Aidha DPP Mganga amesema kufuatia tukio hilo rais John Pombe Magufuli ameagiza hatu kali za kisheria zichukuliwe kwa waliohusika ili kukomesha tabia hizo zinazoichafua serikali kwa wananchi wake na dunia nzima
Chanzo: ITV
DPP afuta kesi ya mauaji iliyokuwa ikimkabili mfanyabishara wa Tabora kwa madai alibambikiwa
Reviewed by Zero Degree
on
3/16/2019 07:50:00 AM
Rating:
Reviewed by Zero Degree
on
3/16/2019 07:50:00 AM
Rating:
