Ngorongoro Heroes yatwaa ubingwa Cecafa U20, Kelvin John atikisa Afrika Mashariki
Bao hilo pekee limepatikana mnamo dakika ya 45 ya kipindi cha kwanza kwa Otieno Onyango kujifunga.
Ushindi huo unaipa rasmi Tanzania kikombe hicho ambacho mashindano yake yalikuwa yanafanyika nchini Uganda.
Baada ya ushindi huo, Ngorongoro wanatarajia kurejea nchini kuanzia kesho.
Ushindi huo unaipa rasmi Tanzania kikombe hicho ambacho mashindano yake yalikuwa yanafanyika nchini Uganda.
Baada ya ushindi huo, Ngorongoro wanatarajia kurejea nchini kuanzia kesho.
Kelvin John ameibuka mchezaji bora wa mashindano hayo |
Mshambuliaji Kelvin John wa timu ya taifa ya vijana chini ya miaka 20, Ngorongoro Heroes, ameibuka mchezaji bora wa mashindano na mfungaji bora, akiwa amefunga goli 7 kwenye mashindano ya CECAFA U20.
Akizungumza baada ya mchezo wa fainali ambapo Tanzania U20 imeifunga Kenya U20 goli 1-0, Kelvin amesema kocha Zuberi Katwila alilkuwa anawaanda vizuri kwenye kila mechi.
Aidha Kelvina ameweka wazi kuwa anampenda nahodha wa Taifa Stars Mbwana Samatta kwasababu amefanikiwa na yeye anatamani kuwa kama yeye.
Ngorongoro Heroes yatwaa ubingwa Cecafa U20, Kelvin John atikisa Afrika Mashariki
Reviewed by Zero Degree
on
10/05/2019 06:20:00 PM
Rating: