Loading...

UN kutaja mataifa yanayochafua mazingira


Inadaiwa kuwa joto limeongezeka kwa zaidi ya kipimo cha nyuzi joto mbili, na kuhatarisha zaidi sayari ya dunia.

Hayo ni kwa mujibu wa ripoti mpya inayotarajiwa kutangazwa na Umoja wa Mataifa.
Image copyrightEPA
Image captionJoto limeongezeka kwa zaidi ya kipimo cha nyuzi joto mbili, na kuhatarisha zaidi sayari ya dunia
Umoja huo unatarajia kuchapisha mpango mpya wa kukabiliana na mabadiliko ya hali ya hewa duniani.
Mpango huo umewasilishwa na mataifa 146, yanapojiandaa kushughulikia mabadiliko ya hali ya hewa.
Image captionMpango huo umewasilishwa na mataifa 146, yanapojiandaa kushughulikia mabadiliko ya hali ya hewa
Ripoti hiyo inatazamiwa kuelezea kwa mapana na marefu zaidi hali ya sasa ya mazingira katika mataifa ambayo hayataweza kuzuia kuongezeka kwa kiwango cha joto kwa sasa duniani.
Umoja huo vilevile unatarajiwa kuelezea waziwazi mataifa kadhaa tajiri au maskini ambayo yamesaidia kupunguza hewa chafu ya Carbon Dioxide.
UN kutaja mataifa yanayochafua mazingira UN kutaja mataifa yanayochafua mazingira Reviewed by Zero Degree on 10/31/2015 07:39:00 AM Rating: 5

Powered by Blogger.