Loading...

Ufisadi mwingine waibuliwa bandarini Dar [ Serikali yapoteza jumla ya Sh 48.47 bilioni ].

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

Serikali imepoteza jumla ya Sh48.47bilioni baada ya makontena 11,884 na magari 2,019 kupitishwa badarini Dar es Salaam bila kulipiwa kodi.



Hata hivyo, jumla ya watu saba wanashikiliwa na wengine nane wanatafutwa na Jeshi la Polisi kwa kuhusishwa na ukwepaji kodi huo uliolikosesha taifa mapato.

Akizungumza na wanahabari leo jijini Dar es Salaam, Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa amesema ufisadi huo umebainika baada ya serikali kuzifanyia ukaguzi bandari zote za nchi kavu (ICDs) jijini Dar es Salaam.


Akifafanua, Waziri Mbarawa amesema makontena hayo 11,884 yalikuwa na thamani ya Sh 47.4 bilioni wakati magari gari 2019 zenye thamani ya sh 1.07bilioni yalitolewa bandarini pasipo kulipiwa tozo.


Credits: Mwananchi


Comment & Share this story!!
Ufisadi mwingine waibuliwa bandarini Dar [ Serikali yapoteza jumla ya Sh 48.47 bilioni ]. Ufisadi mwingine waibuliwa bandarini Dar [ Serikali yapoteza jumla ya Sh 48.47 bilioni ]. Reviewed by Zero Degree on 12/29/2015 03:14:00 PM Rating: 5

Powered by Blogger.