Loading...

Ugonjwa wa ajabu wazidi kushika kasi mkoani Dodoma.


Mgonjwa mmoja aliyekuwa akiugua ugonjwa wa ajabu, ulioukumba mkoa wa Dodoma, amefariki na kufanya idadi ya waliokufa kwa ugonjwa huo kufikia saba huku wanaougua wakiongezeka na kufikia 21, kati ya hao wawili ambao ni watoto wakiwa katika hali mbaya.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu alisema hayo mjini hapa jana alipotoa taarifa kuhusu hali ya ugonjwa huo na hatua ambazo serikali imekuwa ikichukua kukabiliana nao.

Ugonjwa huo kwa mjibu wa Ummy, ulianzia katika wilaya ya Chemba ambako watu tisa wa familia moja kutoka kijiji cha Mwaikisabe kata ya Kihama, waliathirika na baadaye wagonjwa wengine walianza kupatikana kutoka vijiji vya karibu.

Dalili za ugonjwa huo zilionekana kuwa ni kutapika, kuharisha, kupata rangi ya manjano machoni, kuwa na maumivu ya tumbo na kuvimba tumbo kwa kujaa maji katika muda mfupi, lakini hawapati joto kali wala harara katika ngozi.

Taarifa za awali za chanzo cha ugonjwa huo kwa mujibu wa Waziri, ilitajwa kuwa ni watu hao kula nyama ya ng’ombe aliyechinjwa baada ya kuvunjika mguu, ingawa baaadhi ya watu waliokula nyama ya ng’ombe huyo hawajaugua.

Source: Mtembezi
ZeroDegree.
Ugonjwa wa ajabu wazidi kushika kasi mkoani Dodoma. Ugonjwa wa ajabu wazidi kushika kasi mkoani Dodoma. Reviewed by Zero Degree on 6/20/2016 11:17:00 AM Rating: 5

Powered by Blogger.