Loading...

Balozi Sefue afunguka

Katibu Mkuu Kiongozi mstaafu, Balozi Ombeni Sefue.
  
Dar es Salaam. Katibu Mkuu Kiongozi mstaafu, Balozi Ombeni Sefue amesema baada ya miaka mingi ya utumishi wa umma sasa ni wakati wake wa kupumzika na hafikirii kujitosa katika siasa.

Balozi Sefue ambaye alikuwa kivutio kwenye televisheni kutokana na kutoa taarifa za kutenguliwa uteuzi kwa watumishi waandamizi wa umma kabla ya kibao kumgeukia, amesisitiza kuwa siasa haipo katika damu na kwamba kazi anayopenda ni kuzisaidia taasisi za ujenzi kwa kuwa ni taaluma anayoipenda.

Mbali na kuonyesha kutokuwa na mpango huo, Balozi Sefue aliupongeza utendaji kazi wa Serikali ya Awamu ya Tano kwa maelezo kuwa una kasi nzuri na kwamba kurejea kwa uadilifu ni jambo linalomfurahisha zaidi akiwataka vijana kufanya kazi kwa bidii baada ya kuaminiwa na kupewa nafasi mbalimbali.

Balozi Sefue ambaye awali hakuonekana kuwa mmoja wa watu ambao wangeng’olewa kwa sababu yoyote ile, alilazimika kuondoka Ikulu ndani ya siku 123 tangu Rais Magufuli aapishwe kuwa Rais na siku 67 tangu balozi huyo atangazwe kuendelea na wadhifa wake. Uteuzi wake ulitenguliwa Machi 6 na nafasi yake kuchukuliwa na Balozi John Kijazi.

Baada ya kimya cha muda mrefu, Mei mwaka huu, Katibu Mkuu Ofisi ya Rais (Utumishi wa Utawala Bora), Dk Laurean Ndumbaro alikaririwa akisema kuwa baadhi makatibu wakuu walioachwa katika uteuzi na Rais, wapo waliostaafu kwa mujibu wa sheria, akiwamo Balozi Sefue.


Source: Mwananchi
ZeroDegree.
Balozi Sefue afunguka Balozi Sefue afunguka Reviewed by Zero Degree on 7/16/2016 09:59:00 AM Rating: 5

Powered by Blogger.