Loading...

Klabu ya Simba kumsajili mshambuliaji wa kimataifa wa Ivory Coast, Kipre Tchetche.

MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Ivory Coast, Kipre Tchetche huenda akaichezea klabu ya Simba msimu ujao baada ya uongozi
wa timu hiyo kuwa na mazungumzo ya chini kwa chini na mchezaji huyo aliyefanya vizuri katika msimu minne aliyocheza Ligi ya Tanzania Bara.

Tchetche hajawasili kambini kujiunga na timu yake kwenye maandalizi ya msimu ujao huku uongozi wake ukiwa hauna taarifa zinazomfanya mchezaji huyo kushindwa kujiunga na wenzake kwenye maandalizi hayo.

Akizungumza gazeti hili, Makamu Mwenyekiti wa klabu ya Simba Geofrey Nyange ‘Kaburu’ alisema Tchetche ni mchezaji mzuri na wangependa kuwa naye, lakini hawezi kulizungumzia hilo kwa sababu wapo watu wanaohusika na zoezi la usajili.

“Timu kubwa kama Simba siku zote inahitaji wachezaji wenye kiwango na ubora wa juu kama Tchetche, ukizingatia hiki ni kipindi cha usajili na tupo kwenye mazungumzo na idadi kubwa ya wachezaji ingawa hilo siwezi kulisemea kwa sababu ipo kamati yetu ya usajili inahusika na hilo na itatufahamisha baada ya kukamilisha kazi yake,”alisema Kaburu.

Kiongozi huyo alisema mipango yao kama uongozi ni kuijenga upya timu hiyo kupitia kipindi hiki cha usajili ili kuweza kurudi kwenye ushindani wa mbio za ubingwa kama ilivyokuwa siku za nyuma. Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Azam FC, Nassor Idrissa, alisema wanachojua mchezaji huyo bado ni mali yao kwa sababu bado ana mkataba wa mwaka mmoja kuichezea timu yao, hivyo amezionya timu zinazomhitaji kufuata taratibu na kanuni zinazotakiwa.

“Mimi ningezitaarifu klabu zinazomhitaji Tchetche, ikiwemo Simba ambayo wanatajwa kuja mezani tuweze kujadili na kukubaliana ili tuweze kuwaachia kwa sababu Simba ni watu wetu wa karibu na tumeshafanya nao biashara ya kupeana wachezaji mara kadhaa sijaona kikwazo kinachowafanya washindwe kuja mezani,”alisema Idrissa.

Simba inatajwa kuwa inakaribia kuinasa saini ya Tchetche, wakitaka kutimiza agizo la kocha wake Joseph Omog, ambaye alifanya kazi na mchezaji huyo na kupata mafanikio makubwa katika kipindi cha mwaka mmoja na nusu alichokuwa akiifundisha Azam.


ZeroDegree.
Klabu ya Simba kumsajili mshambuliaji wa kimataifa wa Ivory Coast, Kipre Tchetche. Klabu ya Simba kumsajili mshambuliaji wa kimataifa wa Ivory Coast, Kipre Tchetche. Reviewed by Zero Degree on 7/16/2016 09:37:00 AM Rating: 5

Powered by Blogger.