Loading...

Meya wa Dar apinga Agizo la Makonda.

Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Issaya Mwita Charles.

Yafuatayo ni muhimu kwa wakaaz wa Jiji la Dar kufahamu kama haki yao ya msingi kabla ya utekelezwaji wa amri ya Mh Mkuu wa mkoa wa Dar wa kufanya msako kwenye makazi na nyumba zao.

Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda.

Moja: Kwanza zoezi hili ni BATILI na haliwezi kutekelezeka kwenye Halmashauri zetu za Jiji la Dar es SalaamPili: Nawaomba sasa nielezee sababu ambazo nasema agizo hilo na zoezi hilo litakuwa BATILI :

  1. Sheria ya makosa ya Jinai Inaelezea utaratibu wa kukaguliwa nyumbani kama search warrant ambayo inatolewa Na Mahakama au polisi, Na ambayo Inaelezea wanatafuta nini.
  2. Sheria hiyo pia inamtaka mwananchi kuwakagua maafisa wa Mahakama Na Polisi watakaofika Nyumbani kwake ili wasiweze kumpandikishia ushahidi wa uongo.
  3. Kamwe popote duniani Kibali cha wananchi kukaguliwa majumbani hakiwezi kutolewa Na Viongozi wa kisiasa.
  4. Kwa maagizo hayo inasemekana wananchi watawekwa ndani Kwa kukataa kutii agizo hilo, hakuna sheria Tanzania inayoruhusu Mwananchi kuwekwa ndani kwa sababu za hovyo Kama hizo.

Naomba nimalizie Kwa kusema wananchi wote wa Jiji la Dar wawe na Amani kabisa na wajue haki zao na wajue kuzitetea, sisi viongozi wao tupo imara kusimamia haki zao na maendeleo ya Jiji la Dar es Salaam na Tanzania kwa ujumla.

Issaya Mwita Charles
Mstahiki Meya Jiji la Dar es Salaam.

Source: Mtembezi.
ZeroDegree.
Meya wa Dar apinga Agizo la Makonda. Meya wa Dar apinga Agizo la Makonda. Reviewed by Zero Degree on 7/16/2016 09:26:00 AM Rating: 5

Powered by Blogger.