Loading...

Mkwasa aahirisha kambi Stars.

kocha mkuu wa taifa stars, boniface mkwasa.

KUTOKANA na maombi ya klabu nyingi za Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, kutaka kuandaa wachezaji wao kwa ajili ya msimu ujao, umemlazimu Kocha Mkuu Taifa Stars, Boniface Mkwasa, kuahirisha kambi iliyokuwa ianze Jumatatu Agosti Mosi, mwaka huu, imefahamika.

Klabu ambazo zinaongoza kutoa nyota wengi kwenye kikosi cha Mkwasa ni Simba SC, Young Africans SC, Azam FC na Mtibwa Sugar FC.

Kutokana na hatua hiyo, sasa Mkwasa atakuwa anafuatilia mwenendo wa nyota 24 aliowaita kwenye michezo mbalimbali ya kirafiki ya klabu hizo inayofanyika kabla ya kuanza Ligi Kuu Tanzania Bara (Pre-season matches) na baadaye katika mechi za raundi ya kwanza na pili ya Ligi Kuu kabla ya kukiita tena kikosi hicho kwa ajili ya safari ya kwenda Nigeria.

Taifa Stars ina mechi na Nigeria, ambao utakuwa ni wa kukamilisha ratiba wa Kundi G, utakaopigwa jijini Lagos, Nigeria Septemba 2, mwaka huu, hiyo inatokana na Misri kusonga mbele kufuatia Chad kujitoa. Wachezaji ambao Mkwasa aliwaita mapema wiki hii ni Makipa: Deogratius Munishi Aishi Manula
na Benny Kakolanya.

Mebeki: Kelvin Yondani, Aggrey Morris, Oscar Joshua, Mohamed Husein                         ‘Tshabalala’, Juma Abdul na Erasto Nyoni.

Viungo: Himid Mao, Mohamed Ibrahim, Shiza Kichuya, Jonas Mkude Ibrahim                  Jeba, Mwinyi Kazimoto, Farid Mussa, Juma Mahadhi na Hassan                          Kabunda.

Washambuliaji: Simon Msuva, Joseph Mahundi, Jamal Mnyate, Ibrahim Ajib,                John Bocco na Jeremia Juma.

Credits: IPPMedia
ZeroDegree.
Mkwasa aahirisha kambi Stars.  Mkwasa aahirisha kambi Stars. Reviewed by Zero Degree on 7/31/2016 10:12:00 AM Rating: 5

Powered by Blogger.