Loading...

Madonsela ashinda Tuzo ya Forbes, ampiku Rais Magufuli na Rais Gurib wa Mauritania.

Bi Thuli Madonsela alikabiliana na ufisadi kwa miaka saba Afrika Kusini.
Aliyekuwa mlinzi wa maslahi ya umma nchini Afrika Kusini Thuli Madonsela ametawazwa kuwa mtu mashuhuri zaidi wa Forbes wa mwaka 2016.

Bi Madonsela aliwashinda marais watatu wa Afrika, raia mwenzake wa Afrika Kusini na watu wan chi ya Rwanda katika kushinda tuzo hiyo.

Rais wa Tanzania John Pombe Magufuli na mwenzake Ameenah Gurib wa Mauritania walikuwa wameteuliwa kushindania tuzo hiyo.

Mwingine ni mfanyabiashara wa Afrika Kusini Michiel le Roux ambaye ni mwanzilishi wa benki ya Capitec.

Bi Madonsela, aliyetangazwa mshindi kwenye hafla iliyoandaliwa Nairobi Alhamisi jioni, amejulikana kwa msimamo wake mkali dhidi ya ufisadi alipokuwa anahudumu kama mlinzi wa maslahi ya umma Afrika Kusini. Alihudumu kuanzia mwaka 2009 hadi 14 Oktoba mwaka huu, muhula wa miaka sita.

Kipindi hicho, alimchunguza rais, akawachunguza wakuu wa polisi, maafisa wakuu serikalini na hata wanasiasa wa upinzani.

Uchunguzi wake ulipelekea kusimamishwa kazi kwa mkuu wa polisi Bheki Cele mwaka 2011.

Aliwahi kumchunguza pia kiongozi wa chama cha upinzani cha Economic Freedom Fighters Julius Malema ambaye mwishoni mwa kipindi chake, alimuunga mkono alipofanya uchunguzi kuhusu uhusiano wa Rais Jacob Zuma na familia tajiri ya Gupta.

Alimchunguza pia Rais Zuma kuhusu ukarabati uliofanyiwa makao yake Nkandla.

Bi Madonsela ni mama wa watoto wawili.

Alikuwa wakili na kiongozi wa vyama vya wafanyakazi wakati wa harakati za kupinga utawala wa ubaguzi wa rangi.
Bi Madonsela anasema ufisadi umekithiri sana Afrika Kusini.
Huu ni mwaka wa sita kwa tuzo hiyo ya Forbes kwa mtu mashuhuri zaidi Afrika kutoleewa.

Waliowahi kushinda tuzo hiyo awali ni:

  • 2011 - Sanusi Lamido Sanusi, aliyekuwa wakati huo Gavana wa Benki Kuu ya Nigeria.
  • 2012 - James Mwangi, CEO wa Benki ya Equity, Kenya
  • 2013 - Akinwumi Adesina, aliyekuwa wakati huo Waziri wa Kilimo Nigeria.
  • 2014 - Aliko Dangote, mwenyekiti wa CEO wa kampuni ya Dangote Group, Nigeria.
  • 2015 - Mohammed Dewji, CEO wa kampuni ya MeTL Group, Tanzania

Source: BBC Swahili
ZeroDegree.
Madonsela ashinda Tuzo ya Forbes, ampiku Rais Magufuli na Rais Gurib wa Mauritania. Madonsela ashinda Tuzo ya Forbes, ampiku Rais Magufuli na Rais Gurib wa Mauritania. Reviewed by Zero Degree on 11/18/2016 12:52:00 PM Rating: 5

Powered by Blogger.